UNHCR yalaani shambulio kwenye kambi ya wakimbizi Pakistani
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limelaani na kusikitishwa na shambulio la Alhamisi kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani kaskazini mwa Pakistani. Shambulio hilo kwenye kambi ya Jalozai karibu na Peshawar lilisababisha vifo vya watu Kumi na makumi kadhaa wamejeruhiwa ambapo waathirika hao ni pamoja na wakimbizi na wafanyakazi wa kutoa msaada kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali.