Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ofisi ya Haki za binadamu yazungumzia kujisalimisha kwa Ntaganda

Ofisi ya Haki za binadamu yazungumzia kujisalimisha kwa Ntaganda

Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja ya Mataifa imezungumzia taarifa za kujisalimisha kwa Bosco Ntaganda ambaye anadaiwa kuwa kiongozi wa kikundi cha waasi cha M23 huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC na ambaye anatakiwa na Mahakama ya kimataifa ya uhalifu, ICC.

Msemaji wa ofisi hiyo akimkariri mkuu wa Tume Navi Pillay amesema taarifa zozote zinazoweza kupatikana kwa haki ni za kuungwa mkono. Tarehe 22 mwezi Agosti mwaka 2006 Bosci Ntaganda alituhumiwa na ICC kwa uhalifu wa kivita ikiwemo kuandikisha na kutumia watoto wenye umri wa chini ya miaka 15 kwenye jeshi huko Ituri, jimbo la Orientali kati ya mwaka 2002 na 2003.

Cecile Pouilly ni msemaji wa Tume hiyo ya Umoja wa Mataifa ya Haki za binadamu.

(SAUTI YA POUILLY).

(SAUTI YA POUILLY)

 

(SAUTI YA POUILLY)