Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ushirikiano wahitajika kudhibiti wizi wa haki miliki: WIPO

Ushirikiano wahitajika kudhibiti wizi wa haki miliki: WIPO

Suala la haki miliki linaelezwa kuwa bado linaendelea kuzua utata na kukwamisha matumizi stahili ambayo yanaweza kusaidia nchi kujikwamua kiuchumi.

Barani Afrika ripoti zinaonyesha kuwa mapato mengi hupotea kutokana na kukithiri kwa vitendo vya wizi wa haki miliki, kunafanyika kwenye maeneo mbalimbali.

Ni kwa mantiki hiyo wataalamu wanakutana jijini Dar es Salaam katika mkutano ulioandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa la hakimiliki, WIPO na serikali ya Tanzania. George Njogopa ametuma taarifa hii.