UM kusaidia bara la afrika kudhibiti Haki miliki
Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania na Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Haki Miliki, WIPO Francis Gurry leo wameongoza mkutano kuhusu hakimiliki jijini DSM ukishirikisha wataalamu na viongozi wa serikali na sekta binafsi kutoka zaidi ya nchi 20 barani Afrika kwa ajili ya kujadilia njia bora za kukabiliana na wizi wa haki miliki na namna ya kuchochea ubunifu na ugunduzi. Imeelezwa kuwa kiwango cha wizi wa haki miliki ni cha juu barani afrika, hatua ambayo pia inachochewa na kukosekana kwa sheria na sera zinazolinda kazi za wabunifu na wagunduzi. Kutoka DSM George Njogopa anaarifu zaidi.
(SAUTI YA GEORGE)