Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Tafiti zaidi zahitajika kubaini kiwango cha ukatili wa kijinsia: TAMWA

Tafiti zaidi zahitajika kubaini kiwango cha ukatili wa kijinsia: TAMWA

Siku ya wanawake duniani ni fursa ya kutathmini hatua zilizochukuliwa kulinda hadhi na ustawi wa mwanamke na mtoto wa kike. Nchini Tanzania, chama cha waandishi wa habari wanawake, TAMWA kiliendesha utafiti kubaini kiwango cha ukatili wa kijinsia, utafiti uliofanyika katika wilaya Kumi nchini humo. Je nini kilibainika? Na matokeo ya utafiti huo yanalenga kuboresha nini? Basi ungana na Stella Vuzo wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa mjini Dar es salaam Tanzania katika mahoajiano yake na Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA Valeri Msoka. Valerie anaanza kwa kutaja wilaya husika.