Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNMISS yatoa elimu juu ya kazi na wajibu wa ujumbe huo Sudan Kusini

UNMISS yatoa elimu juu ya kazi na wajibu wa ujumbe huo Sudan Kusini

Katika kutoa elimu juu ya wajibu na majukumu ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa Sudan Kusini (UNMISS) katika jamii ya jimbo la Jonglei, ujumbe huo ulizuru jamii ya watu wa AKUIDENG BOMA, mji ulioko Jalle Payam takribani kilometer 60 kutoka mji unaofahamika kama Bor.

Ungana na Joseph Msami katika makala hii inayomulika juhudi za UNMISS katika kuwaelimisha raia namna ya kushirikiana na ujumbe huo kukomesha mapigano na kuleta amani ambayo imekuwa ni adimu nchini Sudan Kusini, taifa lililozaliwa mwezi Julai mwaka 2011.