Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

EU na FAO zaapa kuunga mkono juhudi za kuhakikisha lishe na usalama wa chakula Malawi

EU na FAO zaapa kuunga mkono juhudi za kuhakikisha lishe na usalama wa chakula Malawi

Rais wa Malawi Joyce Banda amekuwa na mazungumzo na Kamishna wa Maendeleo ya Jumuiya ya Umoja wa Ulaya, Andris Piebalgs, na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la chakula na kilimo FAO José Graziano da Silva, juu ya kukabiliana na tatizo la lishe na ukosefu wa chakula matatizo ambayo yanaendelea kuliandama taifa hilo.

Watendaji hao wa mashirika hayo ya kimataifa wamekuwa na ziara nchini Malawi katika kile kinachoelezea kubainisha mipango ya kulipiga jeki taifa hilo.

Malawi inatajwa kufanya vyema kwenye maeneo ya kukabiliana na tatizo la njaa lakini hata hivyo bado inaandamwa na tatizo la utapiamlo, huku idadi ya watoto waliokubwa na baa hilo ikiongezeka. George Njogopa ana maelezo zaidi

(TAARIFA YA GEORGE