Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Zaidi ya watu milioni nne kukumbwa na uahaba wa chakula Sudan Kusini

Zaidi ya watu milioni nne kukumbwa na uahaba wa chakula Sudan Kusini

Inakadiriwa kuwa karibu watu milioni 4.1 kusini mwa Sudan huenda wakakumbwa na uhaba wa chakula mwaka huu kwa mujibu wa ripoti mpya ya Shirika la kilimo na mazao la Umoja wa Mataifa FAO na lile la mpango wa chakula duniani WFP.

Ripoti hiyo inasema kuwa uzalisaji wa chakula uliongezeka kwa zaidi ya asilia 35 kati ya mwaka 2011 na 2012 kutokana na mvua ya kutosha, ubora wa kilimo na kuongezeka kwa ardhi ya kilimo.

Lakini hata hivyo, asilimia 40 ya watu wa nchi hiyo watakabiliwa na changamoto ya kupata chakula cha kutosha wakati fulani mwaka huu. Joseph Msami na taarifa zaidi

(TAARIFA YA JOSEPH MSAMI)