Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ukabila na udini tishio kwa amani duniani: Dieng

Ukabila na udini tishio kwa amani duniani: Dieng

Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa limehadharishwa kwamba  ongezekeo la uhasama wa vikundi vya kidini na kikabila katika nchi kadhaa linaweza kuchochea ghasia katika nchi hizo.

Akihutubia baraza hilo katika mkutano wa 22 unaoendelea, Mshauri maalum wa Katibu wa Umoja wa Mataifa kuhusu mauaji ya kimbari Adam Dieng amesema nchi zinazokabiliwa na tishio hilo ni Syria,Mali,Sudan,Pakistan,Kyrgstan pamoja na Iraq.

Bwana Dieng ametoa wito kwa Baraza la Haki za Binadamu kutafunjia za  kuzuia tishio hilo kwa sasa ili kuepuka madhara makubwa kwa siku zijazo huku akitolea mifano ya macahafuko yaliyosababishwa na vikundi vya udini na ukabilakatika nchi za  Holocaust, Cambodia, Rwanda, and Sebrenica na kusisitiza kuwa machafuko yaliyotokea katika nchi hizo yanaashiria kushindwa kwa jumuiya ya kimataifa kukomesha ghasia.

SAUTI YA ADAM DIENG