Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makubaliano ya Doha kuhusu Darfur yapewa msukumo

Makubaliano ya Doha kuhusu Darfur yapewa msukumo

Mkutano uliozileta pamoja ujumbe wa pamoja wa Afrika na Umoja wa Maitafa huko Darfur, UNAMID na ofisi ya Umoja wa Mataifa huko Sudan, UNCT umejadili kwa kina njia bora ya kuupa msukumo mpango wa amani katika jimbo la Darfu uliosaniwa Doha, baina ya serikali na kundi la waasi . Mkutano huo umeangazia njia zinazoweza kusaidia kuyapa uhai zaidi makubaliano hayo  ambayo kimsingi yanafungua njia ya kumaliza vita katika jimbi hilo.  Mkutano huo uliofanyika kwenye makao makuu ya UNAID El Fasher, Kaskazini mwa Darfur ulihudhiriwa pia na maafisa shirika la maendeleo ya Umoja wa Mataifa UNDP na ofisi ya uratibu na majanga ya kibinadamu  Taarifa zaidi na George Njogopa.

 (SAUTI YA GEORGE)