Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wahisani watathmini usaidizi wa kibinadamu huko ukanda wa Sahel

Wahisani watathmini usaidizi wa kibinadamu huko ukanda wa Sahel

Mwaka mmoja tangu jumuiya ya kimataifa izindue kampeni mahsusi ya kushughulikia matatizo ya kibinadamu huko Ukanda wa Sahel, hii leo wahisani wamekutana huko Geneva, Uswisi na kutathmini usaidizi huo ambapo wamesema umekuwa wa manufaa lakini bado msaada zaidi wahitajika.

Wakuu wa mashirika ya kimataifa ikiwemo ya Umoja wa Mataifa walitathmini na kusema kuwa usaidizi mkubwa wa dola Bilioni Moja Nukta mbili ulisaidia kuepusha janga la kibinadamu kwa watu Milioni Kumi kweney nchi Nane zilizo ukanda huo wa Sahel barani AFrika. Hata hivyo wamesema mamilioni ya watu bao wanakabiliwa na ukame, ambapo watoto Milioni Moja Na Nusu wenye umri wa chini ya miaka mitano wako hatarini kukumbwa na unyafuzi. Tupate taarifa zaidi kutoka kwa George Njogopa.

(SAUTI YA GEORGE)