Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baraza la Usalama laonya wanaoingilia mchakato wa mpito Yemen

Baraza la Usalama laonya wanaoingilia mchakato wa mpito Yemen

Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeridhia taarifa ya Rais wa baraza hilo kuhusu Yemen ambayo pamoja na kupongeza tangazo la kuwepo kwa mjadala wa kitaifa nchini humo baadaye mwezi huu inaonya wale wote wanaokwamisha mchakato wa mpito nchini humo akiwemo Rais wa zamani Ali Abdullah Salehe.

Akisoma taarifa hiyo kwa waandishi wa habari, Mwakilishi wa kudumu wa Uingereza kwenye Umoja wa Mataifa, Balozi Mark Lyall Grant amesema baraza limeonyesha matumaini kuwa mjadala huo wa kitaifa utawezesha kufanyika kwa kura ya maoni juu ya katiba na hatimaye uchaguzi mwezi Februari mwakani.

Amesema Baraza la usalama limeonya kuwa iwapo vitendo vya kuingilia mchakato wa mpito Yemen utaendelea, Baraza litachukua hatua kwa mujibu wa ibara ya 14 ya katiba iliyoanzisha Umoja wa Mataifa.  Halikadhalika Balozi Grant amesema tarehe Saba mwezi ujao, Uingereza itakuwa mwenyeji wa mkutano wa marafiki wa Yemeni utakaofanyika mjini London.