Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nchi za Asia zajadiliana kuhusu njia za kupunguzwa kwa vichafuzi kwa hewa

Nchi za Asia zajadiliana kuhusu njia za kupunguzwa kwa vichafuzi kwa hewa

Wawakilishi wa serikali kutoka mataifa 19 ya Asia wameanza mikutano mjini Bangkok hii leo inayoandalaiwa na maafisa wa mazingira kutoka nchini Bangladesh na Japan kutafuta mbuni za kupunguza athari za muda mfupi za uchafuzi wa mazingira katika eneo la Asia.

Vichafuzi vya mazingira vikiwemo carbon na Methane vinachangia katika kupanda kwa joto duniani hivi sasa na vinaweza kuwa hatari kwa mazingira na pia kusababisha pia athari ya kiafya kwa binadamu na kilimo. Serikali na maafisa hao wamezungumzia hatua ambazo zinaweza kuchukuliwa kwa haraka kwa maendeleo ya kiuchumi na utunzi wa mazingira. Jason Nyakundi na taarifa kamili.