Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Utupaji na upotevu wa chakula sasa basi: UM

Utupaji na upotevu wa chakula sasa basi: UM

Katika harakati za kuona kuna uhakika wa chakula duniani, kampeni mpya imeanzishwa kuepusha upoteaji au utupaji wa chakula. Kampeni hiyo inayoendeshwa na shirika la chakula na Kilimo duniani, FAO na lile la mazingira, UNEP kwa kushirikiana na wadau wao inazingatia kuwa maelfu ya Tani za chakula hupotea na kusababisha hasara ya dola Trilioni Moja. Je kwa nini hali hii wakati kila uchwao ni kilio cha ukosefu wa chakula? Ungana na Alice Kariuki katika ripoti hii.