Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ukiukaji wa haki za binadamu bado ni changamoto nchini Iraq: UM

Ukiukaji wa haki za binadamu bado ni changamoto nchini Iraq: UM

Suala la haki za binadamu nchini Iraq bado limesalia kuwa changamoto wakati taifa hilo linaposhuhudia mabadiliko kutoka nyakati zilizokuwa na mizozo na ghasia ikielekea kwenye demokrasia na amani imesema ripoti kuhusu haki za binadamu ya shirika la Umoja wa Mataifa.

Ripoti hiyo inasema kuwa suala la ghasia limesalia ajenda kuu huku idadi ya raia waliouawa ikiongezeka ikilinganishwa na wakati kama huo mwaka uliopita. Jason Nyakundi na taarifa kamili.

(SAUTI YA JASON NYAKUNDI)