Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kampuni binafsi za ulinzi nchini Somalia ziongozwe kwa kanuni na sheria : Wataalamu UM

Kampuni binafsi za ulinzi nchini Somalia ziongozwe kwa kanuni na sheria : Wataalamu UM

Wakati Somalia inajenga upya taasisi zake za ulinzi na usalama, serikali ya nchi hiyo imetakiwa kuhakikisha kuwa vikosi binafsi vya ulinzi vinaongozwa kwa kanuni na sheria na havigeuzwi kuwa mbadala wa vikosi thabiti vya polisi.

Hilo ni tamko lililotolewa na kikundi cha wataalamu wanaochunguza matumizi ya mamluki waliofanya ziara nchini Somalia kwa siku saba wakiongozwa na Faiza Patel ambapo walisema kila raia wa Somalia ana haki ya kupatiwa ulinzi na si wale wenye uwezo tu. Taarifa zaidi na George Njogopa.

(SAUTI YA GEORGE NJOGOPA)