Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Idadi ya watalii kwa mwaka 2012 duniani kote leo yafikia Bilioni Moja

Idadi ya watalii kwa mwaka 2012 duniani kote leo yafikia Bilioni Moja

Idadi ya watalii waliotembelea dunia hii leo imetimia Bilioni Moja na kuweka rekodi mpya kwenye utalii wa kimataifa sekta inayochangia nafasi moja kwa kila ajira 12 duniani.

Kwenye tarehe ya kuadhimisha mtalii nambari bilioni moja ambayo ni leo tarehe 13 shirika la utalii duniani UNWTO limetaja hatua ambazo zinaweza kuchukuliwa na watalii kuhahakikisha kuwa safari wanazofanya zinanufaisha wakazi na maeneo wanayozuru.

UNWTO inasema kuwa utalii wa kimataifa umezidi kukua mwaka 2012 hata baada ya kushuhudiwa kwa mdodoro wa kiuchumi. Marcelo Risi ni Afisa Habari mwandamizi wa shirika hilo.

(SAUTI MARCELO)