Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ugonjwa wa kurithi wa Siko Seli nchini Tanzania

Ugonjwa wa kurithi wa Siko Seli nchini Tanzania

Siko seli au seli mundu ni miongoni mwa magonjwa yanayoendelea kutikisa nchi mbali mbali duniani ambapo kila mwaka watoto Laki Tatu huzaliwa na ugonjwa huo wa kurithi, na hizo ni takwimu za Shirika la afya duniani, WHO.

Kati ya hao, asilimia 80 wanatoka barani Afrika, ambako Tanzania inashika nafasi ya nne kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa. Nigeria, ni ya kwanza, ikifuatiwa na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na ya tatu ni Angola. WHO inataka nchi yenye tatizo hilo kuweka mpango maalum ili kupunguza ugonjwa huo na hatimaye kuutokomeza.

Je ugonjwa huu huambukizwa vipi? Na Tanzania inachukua hatua gain? Ungana basi na mwandishi wetu kutoka Tanzania, George Njogopa aliyetuandalia makala hii.

(PKG YA GEORGE NJOGOPA)