Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wahamiaji wako hatarini zaidi kuambukizwa Ukimwi: IOM

Wahamiaji wako hatarini zaidi kuambukizwa Ukimwi: IOM

Shirika la kimataifa la Uhamiaji, IOM limesema wahamiaji wanaathirika zaidi na virusi vya ukimwi na Ukimwi hususan katika nchi zenye vipato vya juu.

IOM inasema kuwa ripoti ya mwaka huu ya UNAIDS inaonyesha kuwa kwa mara kwanza katika historia ya Ukimwi, maambukizi mapya ya ugonjwa huo katika nchi zilizokuwa na mzigo mkubwa wa maambukizi hayo yanapungua, lakini bado kuna changamoto.

Ripoti hiyo inatoa mfano wa nchi zenye vipato vya juu kama zile za Amerika Kaskazini na Ulaya ambako inasema idadi ya watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi imeongezeka katika kipindi cha miaka Kumi iliyopita.

Imesema wahamiaji na watu wanaohamahama wako hatarini zaidi kuambukizwa virusi hivyo kwa sababu mipango mingi ya afya huwaengua mara kwa mara na hata hawawezi kupata huduma za afya. Jumbe Omari Jumbe ni msemaji wa IOM

((SAUTI YA JUMBE OMARI JUMBE)