Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Dhuluma dhidi ya wanawake bado yaathiri wanawake 3 kati ya wanawake 10 duniani

Dhuluma dhidi ya wanawake bado yaathiri wanawake 3 kati ya wanawake 10 duniani

Huku siku ya kimataifa ya kupinga dhuluma dhidi ya wake ikitarajiwa kuadhimishwa tarehe 25 mwezi huu Shirika la afya duniani linasema kuwa bado wanawake 3 kati ya wanawake 10 wanapitia dhuluma nyingi duniani. WHO inasema kuwa dhuluma ya kimapenzi ndiyo inayotumika zaidi kama silaha.

WHO Inasema kuwa hata kama upashaji tohara umepungua duniani bado watoto wasichna milioni 2 wako kwenye hatari ya kupashwa tohara. Hata hivyo serikali na mashirika ya umma yanafanya mikakati ya kumaliza dhuluma huyo hasa nchini Kenya ambapo jamii zinashauriwa kukoma kuwapasha tohara wasichana. Dr Marleen Temmerman ni Mkurugenzi mpya kuhusu afya ya uzazi kwenye Shirika la WHO:

(SAUTI YA MARLEEN TEMMERMAN)