Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakimbizi wa Burundi nchini Tanzania waanza safari ya kurejea nyumbani

Wakimbizi wa Burundi nchini Tanzania waanza safari ya kurejea nyumbani

Wakimbizi wa Burundi walioko nchini Tanzania katika kambi ya Mtabila wameanza kurejea nyumbani kutii agizo lilitolewa na serikali ya nchi hiyo ambayo inakusudia kuifunga kambi hiyo ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.

Hadi sasa kiasi cha wakimbizi wapatao 8,9994 wameondoka kwenye kambi hiyo iliyoko mkoani Kigoma na shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na wakimbizi UNHCR linasema kuwa idadi hiyo inaweza kuongezeka katika siku za usoni. Kutoka DSM, George Njogopa anaarifu zaidi.