Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ugonjwa wa Akili nchini Burundi

Ugonjwa wa Akili nchini Burundi

Watalamu wa kimatibabu wanasema magonjwa ya akili ni moja wapo wa maradhi yanayopuuzwa sana, hasa katika nchi zinazoendelea.

Asilimia sabini na tano ya watu wanaokumbwa na magonjwa ya akili wanaishi katika nchi zinazoendelea na wengi wao hawapati matibabu. Mara nyingi, usumbufu wa akili huwapunguzia watu uwezo wa kukabiliana na changamoto za maisha za kila siku, na huchangia mivutano katika familia. Je hali iko vipi nchini Burundi?

Mwandishi wetu wa Bujumbura Ramadhan Kibuga ametembelea mtaa wa Buyenzi mjini humo na kukutana na Mama Iddi anayemlea mwanawe, Idd ambaye anaishi na ugonjwa wa akili na kushuhudia athari mbalimbali za tatizo hilo. Ungana naye kwenye makala haya.

(PKG YA KIBUGA)