Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jopo la wataalamu la Umoja wa Mataifa lasema uzinzi haupaswi kuwa kosa la jinai

Jopo la wataalamu la Umoja wa Mataifa lasema uzinzi haupaswi kuwa kosa la jinai

Jopo la wataalamu huru wa Umoja wa Mataifa linaloshughulikia suala la unyanyasaji dhidi ya wanawake kisheria na kimatendo limezitaka serikali kufuta sheria zote zinazotambua uzinzi kuwa kosa la jinai na kuweka adhabu kama vile faini, kifo kwa kunyongwa au kupigwa mawe.

Mkuu wa jopo hilo linalokutana mjini Geneva, Uswisi Kamala Chandrakirana amesema uzinzi haupaswi kabisa kubainishwa kuwa kosa la jinai huku akigusia ubaguzi wa adhabu hizo baina ya wanawake na wanaume.