Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Idadi ya watu wanaokimbia makazi yao Myanmar bado yaongezeka: UNHCR

Idadi ya watu wanaokimbia makazi yao Myanmar bado yaongezeka: UNHCR

Nchini Myanmar,  idadi ya watu wanaokimbia makazi yao kwa ajili ya kutafuta chakula, huduma za afya, makazi na misaada mingine inazidi kuongezeka ikiwa ni miezi minne tangu kutokea kwa vurugu baina ya jamii tofauti kwenye jimbo la Rakhine, magharibi mwa nchi hiyo.

Takwimu zilizotolewa na mamlaka katika eneo hilo zimeonyesha kuwa hivi sasa kuna watu Elfu Sabini na Watano walio katika makambi kwenye jimbo la Rakhine, katika vitongoji vya Sittwe, Kyauk Taw na Maungdaw.

Idadi hiyo ni kubwa ikilinganishwa na makadirio ya awali ya serikali ya watu Elfu Hamsini iliyotolewa baada ya vurugu mwezi Juni mwaka huu: