Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Syria yadai kutumwa kwa magaidi nchini humo

Syria yadai kutumwa kwa magaidi nchini humo

Serikali ya Syria imeishutumu ripoti ya hivi majuzi ya tume huru ya kimataifa inayochunguza ukiukaji wa haki za binadamu nchini humo na kuitaja kuwa isiyo sahihi. Serikali ya Syria inadai kuwa ripoti hiyo ina ushahidi usiokuwa wa kweli.

Kupitia taarifa kwa baraza la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa balozi wa Syria mjini Geneva Faysal Khabbaz Hamoui ameshutumu baadhi yamataifa jirani wa Syria akisema kuwa wanataka mzozo uliopo nchini mwake undelee kwa kuyapa silaha na mafunzo makundi ya upinzani. Hamoui amesema kiwa vikwanzo ilivyowekewa Syria sio tu vimechangia kudorora kwa hali ya kibinadamu nchini humo bali pia ni tishio kwa uhuru wake.

(SAUTI YA FAYSAL KHABBBAZ)