Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wakimbizi zaidi kutoka Syria waendelea kuwasili nchini Lebanon

Wakimbizi zaidi kutoka Syria waendelea kuwasili nchini Lebanon

Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa linasema kuwa kuna ongezeko kwa wakimbizi kutoka Syria wanaowasili mashariki bonde la Bekaa nchini Lebanon ikikadiriwa kuwa takriban watu 2,200 wamewasili eneo hilo juma lililopita. Hata hivyo wakimbizi wanaowasili kaskazini mwa Lebanon wamesalia kuwa ni watu 400 wanaowasili kila siku.

UNHCR inaweka laini mpya za simu ili kuwawezesha wakimbizi wanaoendelea kuongezeka wanaohitaji kujiandikisha. Msukosuko ulioshuhudiwa wiki iliyopita haukuwaruhusu wakimbizi kujiandikisha. UNHCR pia inachunguza hali ya wakimbizi katika eneo la Akkar ambalo hadi sasa linakumbwa na mashambuilizi kutoka Syria . Adrian Edward ni msemaji wa UNHCR.

(SAUTI YA ADRIAN EDWARD)