Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashirika ya kutetea haki za binadamu yaitaka serikali ya Tanzania kulifungulia gazeti

Mashirika ya kutetea haki za binadamu yaitaka serikali ya Tanzania kulifungulia gazeti

Mashirika ya kutetea haki za binadamu nchini Tanzania yameikosoa serikali kwa jinsi inavyotendea  uhuru wa vyombo vya habari na wakati huo huo yametoa siku saba kwa serikali hiyo kulifungulia gazeti moja ililolifungia vinginevyo yataanzisha maandamano ya amani nchi nzima.

Mashirika hayo ni yale yanayotetea ustawi wa kijamii yakiwemo kituo cha sheria na haki za binadamu, Mtandao wa jinsia TGNP, na taasisi vya vyombo vya habari kusini mwa afrika MISA.

Kutoka DSM, George Njogopa anaarifu zaidi