Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNESCO na PAMP kuzindua shughuli ya ukusanyaji wa safaru na medali

UNESCO na PAMP kuzindua shughuli ya ukusanyaji wa safaru na medali

Shughuli ya shirika la sayansi na utamadunia la Umoja wa Mataifa ya kukusanya sarafu na medali itaaanza kote duniani kupitia makubalino kati ya shirika la elimu, sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO na kampuni ya kuosha madini ya PAMP S.A.

Programu hiyo mpya itasaidia kukusanya sarafu na medali zilizotengezwa kwenye nchi binafsi na zilizo na picha za sehemu za kitamaduni zilizo kwenye orodha ya UNESCO kote duniani. Kupitia ushirikino wa benki kuu, PAMP S.A itaongoza usambazaji wa sarafu hizo kama moja ya njia ya kusherehea mafanikio ya shirika la UNESCO kwenye masuala ya sayansi , elimu na utamaduni.