Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mamia ya watu wanaendelea kuhama nchini Syria kila siku kunapoendelea kushudiwa mapigano:UNHCR

Mamia ya watu wanaendelea kuhama nchini Syria kila siku kunapoendelea kushudiwa mapigano:UNHCR

Huku ghasia zikiendelea kuchacha nchini Syria watu zaidi wanaendelea kuhama makwao kutafuta usalama wao. Takriban watu milioni 1.5 waliohama makwao wamesalia ndani mwa Syria wakitafuta hifadhi kwa familia zingine au kwa makao ya muda. Watu wengine wamekwama wakiwa na hofu na hofu ya kujipata kati kati mwa mapigano au kulengwa wakati wanapohama.

Mji wa Aleppo kwa sasa unakumbwa na msukosuko mkubwa huku misaaada ya kibinadamu ikihitajika kwa dharura. Takriban shule 45 kwa sasa zinawapa hifadhi watu 7,200 huku idadi ya watu isiyojulikana wakipiga kambi kwenye misskiti . Wafanyikazi wa shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa mjini Aleppo wanasema kuwa hakuna mawasiliano ya mtandao