Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Baada ya kazi nzito naenda kupumzika:Migiro

Baada ya kazi nzito naenda kupumzika:Migiro

Kama tulivyowafahamisha Juma lililopita Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bi Migiro amemaliza muda wake na kurejea nyumbani Afrika baada ya kuutumikia Umoja wa Mataifa kwa miaka mitano.

Migiro alikuwa mwanamke wa pili kushika wadhifa huo na wa kwanza kutoka barani Afrika. Ameondoka akiacha sifa kemkem ya mambo mengi ya kuigwa aliyoyafanya tangu alipoteuliwa mwaka 2007. Akizungumza na mtangazaji wa Idhaa hii Joshua Mmali juma lililopita alieleza mengi aliyofanya, changamoto alizopitia na jinsi alivyoweza kuzikabili.

Leo katika sehemu ya pili anafafanua mchango wake kwa Afrika hususani wanawake, mambo anayojivunia, aliyojifunza katika kazi hii na nini atakifanya nyumbani Afrika baada ya kuwasili. Wasikilize wakianza kujadili suala la afya.

(MAHOJIANO NA BI ASHA ROSE MIGIRO)