UM washirika maonyesha ya saba saba Tanzania
Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania yameingia kwenye maonyesho ya kimataifa ya biashara sabasaba kwa ajili ya kutumia fursa hiyo kuelezea shughuli mbalimbali za Umoja huo nchini humo.
Hii ni mara ya pili kwa Umoja wa Mataifa kushiriki kwenye maonyesho hayo ambayo kilele chake kinafikia tarehe 7 mwezi huu.
Kutoka Dar es Salaam, George Njogopa anaarifu zaidi.
(SAUTI YA GEORGE NJOGOPA)