Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maelfu ya watu bado Wanaishi Kambini nchini Haiti

Maelfu ya watu bado Wanaishi Kambini nchini Haiti

Shirika la kimatiafa la uhamiaji IOM linasema kuwa karibu watu 400,000 bado wamesalia kambini nchini Haiti miaka miwili baada ya taifa hilo kukumbwa na tetemeko kubwa la ardhi. IOM inasema kuwa hata baada ya kupungua kwa idadi ya watu waliohama makwao inahitaji wale ambao bado hawajapata makoa kwenye kambi 575 kushughulikiwa.

Mkurugenzi mkuu wa IOM William Swing ambaye amekuwa akiitembelea Haiti amesema kuwa usalama kwa wanaoishi kambi ndilo suala muhimu hasa kwa wanawake na wasichana walio kwenye hatari ya kudhulumiwa kimapenzi. Jumbe and Omari Jumbe ni msemaji wa IOM.

(SAUTI YA JUMBE OMAR JUMBE)