Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kazi ya kuwa na Dunia Endelevu ndio kwanza Inaanza Rio+20:Ban

Kazi ya kuwa na Dunia Endelevu ndio kwanza Inaanza Rio+20:Ban

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameuambia ulimwengu kwamba ingawa kongamano la kimataifa la Rio+20 limemalizika, lakini kazi ya kujenga dunia endelevu ndio kwanza inaanza.

Ban amekaribisha malengo zaidi ya 700 yaliyotangazwa kwenye mkutano wa Rio na nchi, makampuni ya biashara, bank za maendeleo, vyuo vikuu na mashirika ya Umoja wa Mataifa miongoni mwa wengine, ya kuhakikisha hatua zinachukuliwa kuanzia ngazi za chini. Ahadi kadha wa kadha zimetolewa katika mkutano huo na sehemu kubwa ya jumla ya dola zaidi ya bilioni 513 zilizoahidiwa inagusa maeneo ya usafiri, nishati, elimu na uundwaji wa ajira zinazojali mazingira. Pia watu wameonyesha ari ya kujitolea.

(SAUTI YA BAN KI-MOON)