Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Duru ya mwisho mjadala wa Rio+20 imeanza Brazil

Duru ya mwisho mjadala wa Rio+20 imeanza Brazil

Majadiliano ya matokeo ya mwisho ya mkutano wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo endelevu au Rio+20 yako yako katika hata za mwisho.

Majadiliano hayo yanaanza rasmi Juni 20 hadi 22 mjini Rio Dejaneiro Brazili ambako wakuu wan chi na serikali mbalimbali wanatarajiwa kutia saini nyaraka muhimu kwenye mkutano huo.

Mkutano huo pia unahudhuriwa na makundi mbalimbali, wakiwemo wadau wa maendeleo, jumiya ya kidini, wawakilishi wa jumuiya za kijamii na mashirika yasiyo ya kiserikali yaani NGO’s.

Winnie Kodi kutoka Sdan anawakilisha NGO iitwayo Delibaya Nuba Womens Development Organisation ambayo inatetea haki za wanawake.

(MAHOJIANO NA WINIE KODI)