Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Afisa wa masuala ya Haki za Binadamu wa UM yuko ziarani Burundi

Afisa wa masuala ya Haki za Binadamu wa UM yuko ziarani Burundi

Afisa wa Umoja wa Mataifa anayehusika na masuala ya haki za binadamu Ivan Simonovic leo ameanza ziara nchini Burundi ili kutathimini hali ya haki za binadamu katika taifa hilo lililotawaliwa na vita kwa muda mrefu na ambalo liko katika juhudi za kuanzisha hivi karibni tume ya ukweli na maridhiano.

Baada ya kutoka Burundi afisa huyo ataelekea katika taifa jirani la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Mwandishi wetu wa Bujumbura Ramadhani Kibuga anafuatilia zira ya Simonovic na ametuandalia ripoti hii.

(RIPOTI YA RAMADHAN KIBUGA)