Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Umoja wa Mataifa una mpango wa kukusanya dola milioni 180 kufadhili

Umoja wa Mataifa una mpango wa kukusanya dola milioni 180 kufadhili

Katika mswada wa mpango huo ulioandaliwa na ofisi ya Umoja wa mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu OCHA Wasyria milioni moja wanahitaji msaada wa dharura Syria, hata hiyo uongozi wa Syria bado haujaidhinisha mpango huo.

Akizungumza mjini Geneva mkurugenzi wa operesheni wa OCHA John Ging amesikitika kwamba ucheleweshaji wa kuidhinisha mpango huo unasamabisha adha zaidi kwa watu wa Syria. Bwana Ging amesema huruma iliyoonyeshwa na jumuiya ya kimataifa kwa watu wa Syria sasa itafsiriwe kwa vitendo.

(SAUTI YA JOHN GING)