Zaidi ya watu 100,000 wakimbia mapigano kaskazini magharibi mwa Pakistan
Shirika la kuwahudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limetoa usaidizi kwa maelfu ya familia nchini Pakistan ambazo zimekimbia mapigano kwenye sehemu kadhaa za makabila nchini humo kwenye mpaka kati ya Pakistan na Afghanistan.
Takriban watu 101,160 wengi wakiwa wanawake na watoto wamelazimika kuhama tangu tarehe 20 mwezi Januari wakati vikosi vya serikali vilipoanzisha oparesheni za usalama dhidi ya makundi ya wanamgambo kwenye eneo la Khyber.
(RIPOTI YA GEORGE NJOGOPA)