Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Msafara wa watu wanaorejea nyumbani umekwama katikati ya mapigano Sudan Kusini:IOM

Msafara wa watu wanaorejea nyumbani umekwama katikati ya mapigano Sudan Kusini:IOM

Shirika la wahamiaji la IOM limesema msafara wa magari yanayosafirisha raia wa Sudan Kusini wanaorejea nyumbani kutoka Sudan Kaskazini umekwama katikati ya mapigano kati ya waasi na majeshi ya Sudan Kusini.

Kwa mujibu wa IOM watu zaidi ya 1000 hadi hivi sasa wanashikiliwa. Shirika la IOM limesema linashirikiana na mashirika mengine kuwaokoa raia hao. Jumbe Omar Jumbe anafafanua.

(SAUTI YA JUMBE OMAR JUMBE)