Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ugaidi wa kinyuklia ni tisho kwa dunia:Ban

Ugaidi wa kinyuklia ni tisho kwa dunia:Ban

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema kuwa suala la ugaidi wa nyuklia linatishia usalama wa kimataifa.

Akiongea kwenye mkutano kuhusu usalama wa nyuklia mjini Seoul nchini Korea Kusini Ban amesema kuwa mataifa yote yameungana katika kukabiliana na tisho hili.

Ban pia ana mipango ya kuitisha mkutano wa kimataifa mwezi Septemba  mwaka huu kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjin New York kujadili suala la usalama wa nyuklia.

Martin Nesirky ni msemaji wa Ban.

(SAUTI YA MARTIN NESIRKY)