Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ubaguzi unachochea ghasia:Pillay

Ubaguzi unachochea ghasia:Pillay

Utafiti mmoja unaonyesha kwamba machafuko mengi  yaliyojitokeza katika miaka ya hivi karibuni yamechagizwa vikubwa na hali ya ubaguzi wa rangi.

Utafiti huo unasema kwamba wakati  wa machafuko hayo makundi ya watu wachache hasa wahamiaji ndiyo yanayoathiriwa zaidi.

Kwa mfano utafiti huo umetaja machafuko yaliyotokea mwaka 2007 na 2009 kuwa ni kielelezo sahihi kinachoeleza namna haki za watu zilivyopuuzwa.

Akijadilia hali hiyo kamishna wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Navi Pillay amesema kuendelea kuacha mienendo ya kibaguzi kunatoa tishio kubwa la kuzuka kwa machafuko.