Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mwakilishi wa Katibu Mkuu kuzuru Sudan Kusini

Mwakilishi wa Katibu Mkuu kuzuru Sudan Kusini

Mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu juu ya masuala ya watoto na maeneo yaliyokumbwa na mizozo anatazamiwa kuzuru Sudan Kusini.

Radhika Coomaraswamy anatazamiwa kuwasili nchini humo March 11, na ataaendelea kusalia huko hadi March 17. Katika ziara yake hiyo pia atatembelea jimbo la Jonglei ambalo linaandamwa na machafuko ya kikabila mara kwa mara.

Anatazamia kutupia macho maeneo mbalimbali pamoja na kujionea namna mipango mbalimbali iliyowekwa na serikali yenye shabaha ya kuhakikisha kwamba hakuna mtoto yoyote anayetumikishwa kwenye vikosi SPLM.

Atatathmini athari zilizosababishwa na mapigano ya mipakani baina ya Sudan Kusin na Sudan Khartoum.

Atakuwa na majadiliano na wataalamu mbalimbali watakaoangazia athari zilizosababishwa na vikosi vya waasi wa LRA.