Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ban amtaka rais wa Syria kusitisha mauaji ya raia wake

Ban amtaka rais wa Syria kusitisha mauaji ya raia wake

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amerejea kutoa wito kwa uongozi wa Syria wa kumaliza umwagaji damu unaoendelea nchini humo, na kuongeza kuwa wakati wa utawala wa mtu mmoja na familia kuachizana mamlaka unakwisha.

Amemtaka Rais Al Asad kukomesha ghasia na kusitisha mauaji dhidi ya raia wake. Ban ametoa kali hiyo mjini Beirt Lebanon alipohutubia mkutano wa ngazi ya juu wa mabadiliko na kipindi cha mpito kuelekea demokrasia. George Njogopa anaarifu.

(RIPOTI YA GEORGE NJOGOPA)