Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Bado Sri Lanka inahitaji kujiandaa kwa majanga

Bado Sri Lanka inahitaji kujiandaa kwa majanga

Miaka saba baada ya janga la Tsumani kuikumba Sri Lanka mengi bado yanahitaji kutekelezwa kwa lengo ya kuhakikisha kuwa kunatolewa onyo la mapema. Zaidi ya watu 30,000 waliaga dunia kwenye janga hilo la mwezi Disemba mwaka 2004 ambalo pia lilikumba nchi zingine 13 na kuwaua zaidi ya watu 200,000.

Baada ya janga hilo Sri Lanka ilibuni idara inayohusika na majanga ambayo itatoa onyo la mapema wakati kunapotokea majanga. Monica Morara na taarifa kamili.

 (SAUTI YA MONICA MORARA)