Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maandalizi ya mkutano wa Rio+20

Maandalizi ya mkutano wa Rio+20

Suala la mazingira litaendelea kugonga vichwa vya habari, kwani mwaka 2012 uchumi unaojali mazingira na mkutano wa mazingira wa Rio+20 nchini Brazili vitatawala. Mwaka 2012 pia utakuwa ni mwaka wa nishati endelevu kwa wote, fursa ya upatikaji wake hasa kwa masikini na masikini kabisa. Watu bilioni saba walioko duniani hivi sasa wanahitaji nishati safi, kusoma, kilimo endelevu ili kula na fursa na ajira bora ili kuishi maisha ya hadhi na matumaini.