Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Afisa wa UM alaani machafuko Ivory Coast

Afisa wa UM alaani machafuko Ivory Coast

Afisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa amelaani machafuko yaliyozuka Jumapili Magharibi mwa Ivory Coast na kusababisha vifo vya watu sita na kujeruhi wengine.

Bert Koenders ambaye ni mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu na pia mkuu wa mpango wa kulinda amani Ivory Coast UNOCI ameelezea hofu yake kuhusu machafuko hayo na kusema ni kitendo cha kujutia. Maelezo kamili na Jason Nyakundi.

(RIPOTI YA JASON NYAKUNDI)