Skip to main content

Mlipuko wa bomu Lebanon Kusini wajeruhiwa walinda amani watano wa UM

Mlipuko wa bomu Lebanon Kusini wajeruhiwa walinda amani watano wa UM

Walinda amani watano wa Umoja wa Mataifa nchini Lebanon wamejurhiwa baada ya bomu lililokuwa likilenga gari lao kulipuka Kusini mwa nchi hiyo mapema leo.

Gari hilo la mpango wa Umoja wa Mataila Lebanon UNFIL lilikuwa likisafiri kusini nje kidogo ya mji wa bandari wa Tyre wakati likipolengwa kwa mujibu wa mpango huo.

Walinda amani waliojeruhiwa walipatiwa matibabu katika eneo la tukio na kisha kusafirishwa kwenda kupata matibabu zaidi.

UNFIL inasema timu yake ya uchunguzi hivi sasa inashirikiana na jeshi la Lebanon kupata ukweli na mazingira ya shambulio hilo. UNFIL imekuwepo Lebanon tangu mwaka 1978 na ina walinda amani zaidi ta 12,000 kutoka nchi 35.