Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashambulizi ya mabomu yawaua raia kadhaa nchini Afghanistan

Mashambulizi ya mabomu yawaua raia kadhaa nchini Afghanistan

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan UNAMA umelaani vikali mashambulizi yaliyotokea nchini Afghanistan yaliyowalenga raia hii leo. Raia kadhaa wa Afghanistan waliuawa baada ya mabomu kulipuka kwenye miji ya Kabul na Mazar-j-Sharif.

UNAMA imeyataja mashambulizi hayo kama ya kikatili na yasiyokubalika. Mashambulizi hayo yanajiri baada ya mkutano wa kimataifa uliondaliwa mjini Bonn nchini Ujerumani kujadili  wanajeshi ya kimataifa  ya mwaka 2014 nchini Afghanistan yatakapoondoka .