Mashambulizi ya mabomu yawaua raia kadhaa nchini Afghanistan
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan UNAMA umelaani vikali mashambulizi yaliyotokea nchini Afghanistan yaliyowalenga raia hii leo. Raia kadhaa wa Afghanistan waliuawa baada ya mabomu kulipuka kwenye miji ya Kabul na Mazar-j-Sharif.
UNAMA imeyataja mashambulizi hayo kama ya kikatili na yasiyokubalika. Mashambulizi hayo yanajiri baada ya mkutano wa kimataifa uliondaliwa mjini Bonn nchini Ujerumani kujadili wanajeshi ya kimataifa ya mwaka 2014 nchini Afghanistan yatakapoondoka .