Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wananchi wa DR Congo milioni 32 wapiga kura leo

Wananchi wa DR Congo milioni 32 wapiga kura leo

Wananchi milioni 32 wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo  wameshiriki hii leo katika uchaguzi mkuu ulioshuhudia wagombea 11 wakiwania wadhifa wa urais akiwemo rais anayeondoka madarakani Joseph Kabila na mpinzani wake mkuu Etienne Tchisekedi.

Vilevile wagombea elfu 18 wamejitokeza kuwania nafasi 500 pekee za ubunge. Mwandishi wetu wa maziwa makuu Ramadhani Kibuga amefuatilia siku ya kwanza ya upigaji kura na kutuandalia taarifa hii.

(RIPOTI YA RAMADHAN KIBUGA)