Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Utekelezaji wa sheria za kukomesha ukatili dhidi ya wanawake Afghanistan bado uko mbali:Pillay

Utekelezaji wa sheria za kukomesha ukatili dhidi ya wanawake Afghanistan bado uko mbali:Pillay

 

Maafisa na vyombo vya sheria bado viko mbali katika utekelezaji wa sheria zinazounga mkono usawa na haki za wanawake nchini Afghanistan umesema mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo UNAMA na kamishina mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Navi Pillay. Ripoti iliyotolewa leo inasema serikali ya Afghanistan haijafanikiwa kuzitumia sheria hizo katika kesi nyingi za ukatili dhidi ya wanawake.

Majaji, waendesha mashitaka na polisi katika sehemu nyingi za nchi hiyo wameanza kutumia sheria hizo lakini ni kwa asilimia ndogo. George Njogopa ana taarifa kamili.

(RIPOTI YA GEORGE NJOGOPA)