Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mamia ya wakimbizi wa Ivory Coast na Angola warejea nyumbani:IOM

Mamia ya wakimbizi wa Ivory Coast na Angola warejea nyumbani:IOM

Mamia ya wakimbizi ambao walihama makwao kutokana na mzozo wa uchaguzi ulioikumba Ivory Coast wameanza kurejea nyumbani kwa usaidizi wa shirika la kimataifa la uhamiaji IOM.

Pia shirika hilo  linaendelea kuwasaidia maelfu ya wakimbizi wa Angola walioko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Zambia kurundi nyumbani kwa hiyari yao.

Afisa wa IOM Jumbe Omari Jumbe anafafanua kuhusu jitihada hizo alipozungumza na Monica Morara wa idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa.

(MAHOJIANO NA JUMBE OMARI JUMBE)